Friday, August 19, 2011

SHORT STORY

USALITI WA PENZI.
Siku moja kulikua na Wavulana wawili ambao ni marafiki sana kupita kiasi na Marafiki hawa walikua ni zaidi ya MARAFIKI kwani ni mithili ya NDUGU kwani wanaaminiana kwa kila jambo, Sasa siku moja kati ya story zao walizokua wakizungumza ni pamoja na Kuongea na wapenzi wao kupitia sim kwenye majira ya usiku mmoja kati ya hawa marafiki alianza kuongea na mpenzi wake kwakua siku chache zilizopita walikua hawana maelewano kidogo sasabasi kipindi wanaongea ndipo jamaa huyu alipo hitaji rafiki yake nae amsalimie shemeji yake kwani walikua hawafahamiani na yule shemeji yake ndo kwa mara ya kwanza anamsalimia na kufahamishana vizuri sasa kilichoendelea baada ya kufahamishana ndipo waliendelea na stori nyingine huku wakileteana mzaa ama masihara huku jamaa anasikia tena wakiwa wameweka laudi spika. Baadae ndipo yule msichana anaeongea nae jamaa wa pili ama rafiki wa yule binti{shemeji} msichana alionekana kubadilisha mawazo taratibu na kuhamia kwa shemeji yake bila kutongozwa wala kuambiwa neno NAKUPENDA huku bwana yake akimsikia. Siku ile ikapita akawa hapati kani hewani kama siku mbili hivi ndipo wale marafiki walipoanza kujiuliza inakuwaje yule msichana kumtaka shemeji yake na kumwacha bwana yake isitoshe yeye na shemeji yake huyo aliyetambulishwa hawajuani wala hawajawahi kuonana?. Maswali yaliwaandama bila majibu. Baada ya siku hizo kupita akapatikana tena hewani wale malafiki wakapanga kumjalibu yule msichana kwa kutaka jamaa ambaye ndiye shemeji ampigie yule bint kwa namba yake na wala si ya bwana yake kisha ajifanye kama hayupo nae na aongee nae yeye ili kuona je juzi yake alikosea ama alikusudia kufanya hivyo ndipo alipo mpigia sim huku ikiwa laudi spika pia na msichana akapokea akafahamishwa kua SHEMEJI yako hapa na alimkumbuka na kuanza kuongea nae lakini katika maongezi hayo msichana alionekata kuwa alichokifanya juzi yake usiku alikikusudia haswa wala hakukosea wala kupotea njia alionyesha mkazo wake kua ameshamsahau mpenzi wake na kuanzisha mapenzi mapya kwa shemejiye na kua mpenzi wake badala ya shemeji yake. Jamaa ambaye alikua mpenzi wake aliumia sana lakini alitumia maamuzi ya kiume kuachana nae bila kugombana nae na ambaye alikua mpenzi wake mpya awali alikua shemeji na yeye akaamua kumtosa kwani alijua sio vizuri kua nae atamuumiza rafiki yake pia kwa kujihami na yeye yasije yakamtokea pindi atakavyokua nae. KWELI MAPENZI YANATESA MOYO.

No comments:

Post a Comment